Gigy Money na Mo J Wanatuchezea, Baada ya Vurugu zote zile Sasa Warudisha Mapenzi Kama Zamani

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gigy Money amerudisha penzi kwa aliyekuwa mpenzi wake mtangazaji wa Choice Fm Mo J.

Wiki chache zilizopita Gigy Money na mpenzi wake wa Muda mrefu Mo J walitengeneza headlines za mitandao ya kijamii baada ya kurushiana maneno Kwenye vyombo vya habari.

Baada ya kutibuana mara tu baada ya kujifungua Gigy Money alitangaza kumuacha Mo J huku alisisitiza mtoto sio wake na akimtaja mpenzi wake mpya kuwa baba wa mtoto.

Lakini  mambo yanaonekana shwari kwa sasa kwani  siku ya jana wawili hao walionekana wapi pamoja mara baada ya Gigy kuposti video iliyowaonyesha wakitembea pamoja na mahaba tele.

Na baadae Kupitia ukurasa wake wa Instagram Gigy aliposti picha iliyowaonyesha wawili hao wakiwa nisu utupu kuonyesha kwamba wapo vizuri na kusindikiza kwa caption iliyosomekaa “Mzazi mwenzangu 🙈♥“.

Top Post Ad

Below Post Ad