Halima Mdee na John Mnyika Wacharuka Kuhusu Trilioni 1.5 Zilizoibuliwa na GAG


BUNGENI, DODOMA: Wabunge wa CHADEMA, Halima Mdee(Kawe) na John Mnyika(Kibamba) wamemtaka Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango kuwaeleza Watanzania Tsh. Trilioni 1.5 zilizoibuliwa na CAG ziko wapi

Wakizungumza leo Juni 5, wabunge hao wamemtaka CAG kufanya ukaguzi maalumu wa fedha hizo na deni la Taifa huku wakisema kama Dkt. Mpango ameshindwa kuongoza wizara hiyo ni bora akajiuzulu ili asiwe waziri wa fedheha

Halima Mdee naye alipigilia msumari kwa kusema Waziri Mpango anatakiwa ajibu hoja kuhusu Tsh. Trilioni 1.5 na Tsh. Bilioni 200 zilizotajwa kupelekwa Zanzibar ni zipi?

Aidha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, amewataka Wabunge kutojadili suala la Trilion 1.5 ndani ya bunge kutoka kwenye ripoti ya CAG hadi kamati ya PAC itapowasilisha ripoti yake

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad