Hivi Ndivyo Irene Uwoya na Dogo Janja Walivyoukimbia Mzimu wa Masogange

Hivi Ndivyo Irene Uwoya na Dogo Janja Walivyoukimbia Mzimu wa Masogange
Muigizaji wa filamu Bongo, Irene Uwoya na mumewe, Dogo Janja wamefunguka sababu ya wao kuhama nyumba waliokuwa wakiishi hapo awali.

Dogo Janja amesema wamelazimika kuhama nyumba hiyo na kwenda kupanga nyumba nyingine ambayo hulipa US Dollar 800 kwa mwezi kutokana na umbali, pili mkewe, Irene alikuwa akisumbuliwa na kumbumbuka za mara kwa mara kuhusu marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’.

“Nahisi kama nilikuwa namuona hivi, kwa hiyo nikashindwa, eeeh!! mara nyingi pia nahisi kama anapita hivi,” amesema Irene Uwoya.

“Of cause inaweza kuwa sababu kila akijitahidi inashindikana kwa sababu alikuwa ni mtu tumemzoea sana,” Dogo Janja ameiambia Clouds FM.

Marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ alifariki April 20, 2018 katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar es Salaam, alikuwa rafiki wa karibu sana na Irene Uwoya.

Top Post Ad

Below Post Ad