Huddah Afunguka Uhusiano Wake na Daimond

Huddah Afunguka Uhusiano Wake na Daimond
Mrembo kutokea nchini Kenya, Huddah Monroe amefunguka sababu za ukaribu wake na label ya WCB.

Huddah katika mahojiano na The Playlist ya Times FM amesema kuwa ukiachilia mbali sababu za kibiashara, amekuwa akivutiwa na uchapakazi wa timu nzima ya WCB.

“The vibe is, WCB napenda sana ni watu wanajima, watu wana njaa ya maisha , so for me WCB have the some kind of vibe the i have. Wanapenda maisha mazuri, so they very work hard hawalalai saa 24 wapo kwenye kazi, so that I like that,” amesema Huddah.

Huddah Monroe yupo nchini Tanzania kwa ajiili ya ku-host show ya Harmonize inayofanyika siku ya leo June 16, 2018. Utakumbuka mwishoni mwa mwaka 2016 Huddah alishindwa kufika katika show ‘Wasafi Beach Party’ kwa kile alichodai ni kushindwa kufikia makubaliano kati yake na Diamond.

Top Post Ad

Below Post Ad