Makombe 8 Bandia ya Kombe la Dunia Yakamatwa Yakiwa Yamejazwa Misoko ya Bangi na Cocaine

Makombe 8 Bandia ya Kombe la Dunia Yakamatwa Yakiwa Yamejazwa Misoko ya Bangi na Cocaine
Nchini Argentina yamekamatwa makombe 8 bandia yenye muonekano sawa na ule wa Kombe la Dunia yakiwa yamejazwa misokoto ya bangi na Cocaine.



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa katika Gazeti la The Sun imesema Makombe hayo 8 yamekamatwa Ijumaa ya wiki iliyopita mjini Isidro Casanova katika jimbo la Greater Buenos Aires.

Jeshi la Polisi mjini Isidro Casanova limethibitisha taarifa hizo na tayari watu nane wanashikiliwa kwa tukio hilo na imekadiriwa kuwa kila kombe lilikuwa na mzigo wa Cocaine wenye thamani ya dola $14,819 sawa na Milioni 33.

Top Post Ad

Below Post Ad