Mama Dangote Athibitisha ‘Yeye Ndio Msemaji wa Mwisho Hata Mseme Nini”.

Mama mzazi wa dimaond platinumz amefunguka na kuandika katika ukurasa wake wa instagram amesema kuwa hata isemwe nini lakini pia wanatakiwa wajue kuwa yeye ndio msemaji wa mwisho katika kila kitu na kila anachosema yeye hakiwezi kupingika hata siku moja.

Kama inavyojulikana kuwa katika mitandao ya kijamii sasa hivi mama mzazi wa Diamond Platinumz amekuwa na mgogoro mkubwa na Hamisa Mobeto na mama yake pia kutokana na ukweli kwamba hamtaki Hamisa kuolewa na mtoto wake na kwa sababu yeye hataki anaamini kuwa hakuna anayeweza kupinga hilo.

Kiuhalisia mimi ndio FINAL SAY.. subirienei REALITY SHOW..on @wasafitv ntakavyoweka bayana kila kitu- Aliandika mama yake Diamond.

Top Post Ad

Below Post Ad