Mambo ni Hivi Casto Dickson Achora Tatoo ya Tunda Mkononi

Mambo ni Hivi Casto Dickson Achora Tatoo ya Tunda Mkononi
Moja kati ya penzi ambalo limekuwa likikua kwa kasi ni penzi kati ya Mtangazaji Casto Dickson na Staa Tunda ambao wamekuwa wakionyesha furaha ya penzi lao kwa ku-post picha kwenye mtandao wa Instagram na time hii wawili hao wametuonyesha kukua kwa penzi hilo baada ya Casto kuchora Tattoo ya Tunda.

Casto amechora Tattoo hiyo ya Tunda kwenye mkono wake na wakati wa uchoraji wa Tattoo hiyo wawili hao walikuwa pamoja kwani walianza kupost video na picha zikionesha tukio la uchoraji wa Tattoo hiyo. Je tutegemee naye Tunda atachora Tattoo hiyo..?

Top Post Ad

Below Post Ad