Marekani inaitaka Korea Kaskazini kuangamiza silaha ifikapo 2020

Marekani inaitaka Korea Kaskazini kuangamiza silaha ifikapo 2020
Marekani ina matumaini ya kuanza kuona shughuli ya kuangamizwa silaha nchini Korea Kaskazini ifikapo mwaka 2020, mwa mujibu wa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Mike Pompeo.

Matamshi yake aliyoyatoa alipofanya ziara nchini Korea Kusini, yanafuataia mkutano kati ya Rais Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un.

Trump na Kim Jong Un wakubaliana mambo manne makuu
Walisaini makubaliano ya kufanya kazi katika kuangamiza kabisa silaha za nyuklia katika rasi ya Korea.

Lakini nakala hiyo imekosolewa kwa kukosa taarifa za kina kuhusu ni lini na ni vipi Korea Kaskazini itaachana na silaha zake.

Tags

Top Post Ad

Below Post Ad