Mchezaji Kulipwa 150,000 Kila Mechi Ndondo Cup

Emanuel Memba (kulia) wa Kauzu FC akiwania mpira na beki wa Friends Rangers Mgaya Juma wa Friends Rangers wakati wa mchezo wa nusu fainali ya Ndondo Cup
Mabibo Market kupitia kwa kiongozi wake imeweka wazi kiasi ambacho atalipwa kila mchezaji kwa kila mechi atakayocheza kwenye mashindano ya Ndondo Cup msimu huu.

Naomi Kibago ambaye ni mweka hazina wa Mabibo Market amesema, msimu huu wa Ndondo Cup wamejipanga kulipa ‘kilo na nusu’ kila mchezaji kwa mechi moja.

“Mapato yanaendelea vizuri kama unavyojua hapa sokoni wafanyabiashara wapo wengi hawasumbui kwenye michango kwa hiyo hela ipo.”

“Kila mchezaji atakaechezea Mabibo Market msimu huu tutamlipa Tsh. 150,000 kwa kila mechi na inaweza kupanda zaidi ya hapo.”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad