Mchezaji wa Swansea City Avutiwa na Wimbo wa Chura wa Snura

Mshambuliaji wa klabu ya Swansea City, Wilfried Bony amefunguka kuwa anaupenda wimbo wa Chura wa Snura huku akisifia baadhi ya waigizaji filamu hapa Bongo.

Bony ambaye yupo nchini Tanzania akizungumza na Waandishi wa Habari leo Juni 27, 2018 jijini Dar es salaam, amesema kuwa wimbo wa Chura ni wimbo mzuri kusikiliza na video yake inavutia kuitazama hususani kwa wanaume kwani ina wanawake wanaocheza vizuri wimbo huo.

Hata hivyo, wimbo wa Chura mwaka 2016 ulifungiwa na serikali kwa kosa la kukiuka maadili ya Mtanzania rejea kwenye hii link na video hapo chini (Serikali yaufungia wimbo wa Snura ‘Chura’).

Top Post Ad

Below Post Ad