Simba Kiboko Wamchomoa Dida Yanga Wampa Mkataba wa Miaka Miwili

Simba Kiboko Wamchomoa Dida Yanga Wampa Mkataba wa Miaka Miwili
HII ni habari njema kwa mashabiki wa Simba, ni kwamba leo kipa wa zamani wa Yanga, Deogratius Muni­shi ‘Dida’ anasaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba.



Dida awali aliwahi kuwa kipa wa Simba, akaondoka na kwen­da Yanga na baadaye akakimbil­ia Afrika Kusini ambapo alijiunga na timu ya Tucks ya nchi hiyo, ambapo taarifa zilisema kuwa hakuwa anapata nafasi ya kuto­sha ya kucheza.



Hata hivyo, hivi karibuni kipa huyo alitua hapa nchini na taari­fa kusema kuwa anajiunga na timu ya Yanga, Championi likamtafu­ta na ku­zungumza naye ambapo aligoma katakata, lakini habari ambazo tumezi­pata ni kwamba anasaini kuichezea Simba leo.



Chanzo cha ndani cha uhakika kutoka kwenye uon­gozi wa Simba, kimese­ma kuwa Dida atasaini mkataba wa miaka miwili leo ikiwa ni siku moja tu baada ya Meddie Kagere na Pascal Wawa kutua kwenye kikosi hicho cha Msim­bazi.



“Taarifa ni kwamba saa chache zijazo au kesho asubuhi Dida atasaini mkataba wa kuitu­mikia Simba, bado haijafahami­ka ni miaka mingapi kwa kuwa inafanywa siri lakini haiwezi kuwa chini ya miwili kwa kuwa mwenyewe alitaka hivyo.



‘’Analetwa ili kumpa upinzani Aishi Manula na inaonekana kuwa Said Mohammed ‘Nduda’ atapelekwa kwa mkopo kwa msimu ujao kwa kuwa Simba wanaamini kuwa ni kipa mzuri lakini majeraha ndiyo yalimsum­bua msimu uliopita,” kilisema chanzo hicho ambacho kipa karibu na benchi la ufundi la timu hiyo.


Tags

Top Post Ad

Below Post Ad