Zari Awaonya Wasafi Tv Kuwa “ Endapo Mtaendekeza Kiki za Kijinga Mtapotea”

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz Zarinah Hassan ‘Zari’ amekitolea uvivu kituo cha Wasafi Tv.

Bila kujaribu kuwa mmiliki wa kituo hicho cha habari ni Diamond, Zari amewajia juu akiwataka kuripoti Habari za maana kuhusu mambo yanayoendelea nchini.

Zari alitoa povu hilo baada ya Wasafi Tv kuposti clip ya kipindi cha Refresh kinachorushwa na kituo hiko kikionyesha mahojiano waliyofanya na video Queen maarufu Irene Au Lynn.

Kwenye mahojiano hayo Irene aliulizwa endapo anamfahamu Zari ambapo alijibu kuwa hamjui Zari wa hajawahi kumsikia ambapo alisikika akisema ‘Zari Who?’.

Baada ya clip hiyo kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii Zari alienda kwenye ukurasa wa kituo hicho na kuwataka waripoti mambo ya maaan yanayoendelea Kwenye jamii badala ya kukazania mambo ya kijinga.

Top Post Ad

Below Post Ad