Jua Layeyusha Barabara ya Lami Australia

Jua Layeyusha Barabara ya Lami Australia
Wenye magari katika eneo moja nchini Australia wamelazimika kuyaacha magari yao baada ya lami kuanza kuyeyuka barabarani.

Tairi za magari ziliharibiwa vibaya na lami na sasa madereva takriban 50 wanadai fidia.

"Sijawahi kuliona jambo kama hili maishani na taarifa zilipoaza kutolewa jana, lilikuwa jambo la kushangaza sana," meya wa eneo hilo Joe Paronella ameambia ABC.

Maafisa wanasema kisa hicho kilisababishwa na jua kali, pamoja na hali kwamba ukarabati ulikuwa umefanyika wiki iliyopita.

Barabara hiyo inapatikana katika eneo la Atherton Tablelands kusini mwa mji wa Cairns na ilifungwa kwa muda.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad