Manara amkumbusha Kessy jinsi alivyoondoka Simba


July 27 2018 club ya Yanga ilitoa list ya wachezaji itakaowatumia msimu wa 2018/2019 hiyo ni baada ya siku moja dirisha la usajili la Ligi Kuu kufungwa, Yanga walitoa list hiyo na kutaja majina ya wachezaji wanne walioachana nao. 

Kati ya hao yupo Hassan Kessy ambaye awali iliripotiwa kuwa amepata timu nchini Zambia, ila kumbe Yanga na Hassan Kessy indaiwa kuwa hawakufikia makubaliano na hatimae wakaja kumpa taarifa za kutomsajili dakika za mwisho. 

Baada ya taarifa hizo kutoka unajua Kessy aliwahi kucheza Simba pia lakini inadaiwa hakuondoka vizuri hivyo afisa habari wa Simba SC Haji Manara akaandika ujumbe huu kupitia ukurasa wake wa instagram kuhusiana na malalamiko ya beki huyo. 

“Baadhi ya Binaadam hujisahau sana..huwa wanakosa utu na hisani…kila siku nasema hivi Vilabu vina mila zake na mifumo yake lazma uviheshimu..Dogo uliondoka kwetu kwa kejeli sana.ukaongea kila aina ya maudhi hukutosheka” 

“Ukashuka kwenye basi mkiwa na kombe pale Msimbazi ukatubeza mno..cc hatukukujibu..leo kiko wapi?mwenzio Ajibu kahama kimya kimya….Huyo ndio Mungu na hizi ndio Simba na Yanga!! 
But cc tunaendelea kukutakia kheri huko uendako,"
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad