Mbowe Atoa Msimamo Wake juu ya CHADEMA


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ameagiza uongozi wa chama hicho kila wilaya kujenga ofisi ifikapo mwaka 2020 na kuondokana na adha ya kupanga.


Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe akiweka jiwe la msingi kwenye jengo la ofisi ya Chama hicho Wilayani Tarime.

Mbowe amesema hayo leo Jumapili Julai 29, 2018 wakati akiweka jiwe la msingi katika jengo la ofisi ya Chadema wilayani Tarime mkoani Mara, ambapo amesisitiza kuwa mpango ujenzi wa ofisi hizo ulicheleweshwa na huu haukuwa muda wake.

“Mpango wa ujenzi wa hili jengo umecheleweshwa na huu haukuwa muda wake lakini nawapongeza  viongozi walioona njozi ya kuanzisha ujenzi huu ambao uko hatua ya renta ili kuunga mkono ujenzi huu Mimi naanza na Shilingi milioni mbili kila mbunge mkoani Mara achangie milioni moja," amesema Mbowe.

Mbowe  ametoa maagizo hayo wilayani humo ambapo amekwenda kwaajili ya uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Turwa ambao umefanyika leo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad