Mganga wa Kienyeji Aliyempa Nguvu ya Kujikinga na Risasi Auawa kwa Kupigwa na Risasi na Mteja Wake

Mganga wa Kienyeji Aliyempa Nguvu ya Kujikinga na Risasi Auawa kwa Kupigwa na Risasi na Mteja W
 Mganga wa kienyeji aitwae Chinaka Adoezuwe mwenye miaka 26 Raia wa Nigeria aliyedai kuwa ana nguvu za kuzuia risasi ameuawa kwa kupigwa na risasi na mteja wake.

Inadaiwa kuwa Mganga huyo ambaye alikuwa akijinasibu kuwa ana uwezo kuzuia risasi alimuagiza mteja wake ampige risasi wakati akiwa anavaa dawa hizo za kuzuia risasi shingoni ili kumthibitishia mteja wake kuwa ana uwezo huo kitu ambacho kilipelekea kukatisha uhai wake.

Kwa upande mwingine jeshi la Polisi nchini humo limemkamata mteja huyo kwa madai ya mauaji na anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Aidha imeelezwa kuwa kwa siku za hivi karibuni nchini Nigeria kumetokea Waganga wengi wanaodai kuwa wana nguvu za kuzuia risasi.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad