Mwanamume akwama baada ya lami kuyeyuka barabarani Newcastle, Uingereza

Mwanamume mmoja nchini Uingereza amewashangaza wengi baada ya kukwama kwenye lami iliyokuwa imeyeyuka katika barabara moja akielekea dukani kununua staftahi.

Kijana huyo wa miaka 24 aliwapigia maafisa wa huduma za dharura kupitia nambari 999 baada ya mguu wake wa kushoto kukwama barabarani.

Mguu wake ulikuwa umetumbukia hadi karibu pajani katika barabara moja ya pembeni eneo la Heaton, Newcastle.

Maafisa wa huduma za dharura walilazimika kuchimbua barabara eneo alipokuwa amekwama wakitumia nyundo na patasi kuutoa mguu wake.

Wanasema alinusurika bila jeraha kutokana na hali kwamba alikuwa amevalia "buti la babu yake aina ya Dr Martens" ambazo hufika hadi magotini.



Msemaji wa zima moto amesema tukio hilo lilisababishwa na jua kali ambalo limekuwa likiwaka eneo hilo.

Amesema: "Wakati kuna jua, tahadhari mambo kama haya yanaweza kutokea - kuweni makini zaidi hasa mnapotembea."

Kisa hicho kimetokea siku chache baada ya lori la kusafirisha taka kudidimia kwenye barabara moja ya lami Newbury, Berkshire.

Watu wametahadharishwa kuwa makini hasa wanapotembea Maeneo mengi kaskazini na kusini mwa dunia yamekuwa yakishuhudia jua kali.

Lami yayeyuka Queensland, Australia
Nchini Australia, wenye magari katika eneo la Atherton Tablelands jimbo la Queensland walilazimika kuyaacha magari yao baada ya lami kuanza kuyeyuka barabarani.

Tairi za magari ziliharibiwa vibaya na lami na sasa madereva takriban 50 wanadai fidia.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad