Nay wa Mitego Awaacha Watu Njia Panda

Nay wa Mitego Awaacha Watu Njia Panda
Hili linaweza likawa la kushangaza kutoka kwa staa wa Bongo Fleva Nay wa Mitego baada ya kuweka wazi kuwa kwa sasa yupo single ikiwa hajawahi kuweka mahusiano yake wazi tokea aachane na mzazi mwenzake Siwema japokuwa aliwahi kuhusishwa kutoka na warembo kadhaa.

Nay wa Mitego aliwahi kuhusishwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii Nini miezi kadhaa iliyopita ingawa wawili hao hawakuwahi kukiri kuwa wapo kwenye mahusiano, ila kwa sasa ameweka wazi kuwa yupo single,

Hiki ni kama kitendawili kutoka kwa Nay wa Mitego, je alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na nani? Kupitia instagram account ya Nay wa Mitego aliandika “Usichangie Chochote, Wala Siitaji Comment hata moja , No ushauri wala maoni, yani ni hivyo tu, I’m Single”

Top Post Ad

Below Post Ad