Ofisa habari wa APR Afunguka Tofauti yake na Haji Manara

Ofisa habari wa APR Afunguka Tofauti yake na Haji Manara
Ofisa Habari wa klabu ya APR ya Rwanda, Clever Kazungu, amefunguka na kumuelezea Haji Manara kama mtu mwenye kipaji cha aina yake katika uzungumzaji anapokuwa anawasilisha jambo.

Kazungu amemtaja Manara ambaye ni Ofisa Habari wa Simba akisema ana kipaji cha aina yake katika uzungumzaji huku akisema anamkubali kutokana na kazi anayoifanya kwenye klabu ya Simba.

Kiongozi huyo kutoka APR amemueleza Manara kuwa utofauti wake na yeye kuwa ana uwezo wa kuzungumza maneno mengi huku akisema wanaendana katika kuwasilisha ujumbe kwa umma.

Kazungu amesema Manara anastahili kuwa hivyo kutokana ukubwa wa klabu yake akiamini kuwa pale mtu anapokuwa msemaji wa timu kama Simba ni lazima uwe vile.

Ofisa huyo ambaye pia ni Mwanahabari mkongwe yupo hapa nchini kwa ajili ya michuano ya KAGAME ambapo jana timu yake iliweza kufungwa mabao 2-1 na Simba katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad