Polepole: “Sishangai kutokubalika kwa Rais Magufuli”

Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema kuwa hashangazwi na watanzania wanaopinga jitihada za Rais Magufuli kwani hakuna maendeleo yasiyopitia changamoto.

Akizungumza katika katika  uzinduzi wa ripoti ya pili Twaweza kuhusiana na hali ya siasa nchini Polepole amesema kuwa maneno hayo ni watu wasio na nia ya kumuunga mkono Rais katika muhtasari wa maendeleo ya nchi.

“Sishangai kukubalika kwa Rais kushuka kwani hata kwenye ndoa kuna ‘honeymoon phase’ maendeleo si kitu cha kimiujiza, tunashughulikia maji, umeme, kilimo, miundimbinu’’, amesema Polepole.

Aidha Polepole ameongeza kuwa tafti zinazokuwa zinafanyika bora zilenge zaidi katika kutokomeza umasikini, kupambana na rushwa na kubuni miradi ya maendeleo ili kuunga mkono maendeleo ya taifa.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad