Rais Magufuli ampongeza Mkurugenzi Mkuu wa WFP

Rais John  Magufuli amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Beasley kwa kutembelea Tanzania na dhamira yake njema ya kushirikiana na Tanzania katika kuwasaidia wakulima kuongeza kiwango cha mahindi yanayonunuliwa.

Rais Magufuli amesema Serikali ipo tayari kushirikiana na WFP hasa katika kukabiliana na changamoto ya wakulima kukosa soko la mazao ya ziada na amebainisha kuwa katika msimu huu Tanzania ina takribani tani Milioni 4 za chakula cha ziada kinachopaswa kuuzwa nje ya nchi.

“Namshukuru sana kwa kuunga mkono juhudi tunazozifanya kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania na hii ndio njia pekee ya kuhakikisha nchi inajikomboa kwa kuwa na uchumi wa kweli” Rais Magufuli

“Tumedhamiria kujitegemea na pia namshukuru kwa kuunga mkono ‘Hapa Kazi Tu’ na juhudi zingine zote ikiwemo kupambana na rushwa na kwamba anaiona Tanzania ya pekee na yenye mwelekeo tofauti wa kuleta neema” amesema Rais Magufuli.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad