Rais Trump Ashambuliwa Mitandaoni kwa Kukosea Kiingereza

Rais wa Marekani, Donald Trump amejikuta akishikwa na hasira baada ya wanaharakati mitandaoni kumsahihisha makosa ya kisarufi (grammatical Error) na kimaandishi (Typing error) kwenye Tweets zake huku wakimkebehi kuwa hajui hata kuandika kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.

Trump ambaye jana Julai 04, 2018 alitwiti mara moja na kisha kufuta twiti hiyo baada ya kushambuliwa kuwa alikosea kuandika, huku akidai mtandaoni kuna vyombo vya habari ambavyo haviangalii anachokifanya bali vinaangalia makosa yake ya kisarufi (grammatical error) mtandaoni.

“Nimeshawahi kuandika vitabu bora na vilivyouzwa zaidi, kwa hiyo huwezi kunipima kamwe kwenye uwezo wangu wa kuandika. Hii inaonesha wazi kuwa kuna vyombo vya habari vinatoa habari bandia (Feki) kwa kutumia muda mrefu kutafuta makosa kwenye tweet zangu,“ameandika Trump kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad