Trump Aikosoa Uingereza Kujitoa Umoja wa Ulaya

Trump Aikosoa Uingereza Kujitoa Umoja wa Ulaya
Rais Donald Trump amesema Uingereza huenda haitapata mikataba ya kibiashara na Marekani iwapo itaendelea mpango wake wa kwa mfumo wa sasa juu ya namna ya kujitenga na Umoja wa Ulaya.

Ameliambia gazeti la Sun kuwa mpango wa huo wa waziri mkuu utaua mipango ya kibiashara ya Uingereza na Marekani,ambapo lengo la Marekani ni kufanya biashara na Uingereza pekee bila kuhusisha umoja wa Ulaya,na ameongeza kuwa Uingereza inapaswa kutoshirikiana kabisa na umoja huo ili kuweza kuiamini na kushirikiana nayo kibiashara.

Bi.Theresa May amekuwa akijitahidi kutumia ziara hii ya kwanza ya Trump kumshawishi biahsra huru kati ya mataifa hayo mawili akisisitiza kwamba suala kujiotoa katika umoja wa Ulaya ni fursa ya kukukuza uchumi wa Marekani na Uingereza.

Katika hatua nyingine rais Trump amemsifia aliyekuwa waziri wa mambo wa nje alijiuzuru Boris Johnson na kudai kuwa anafaa hata kuwa waziri mkuu lakini wamempoteza.

Ameongeza kuwa kile kinachoendelea kwa sasa katika Uingereza kujitoa katika umoja huo wa Ulaya ni tofauti kabisa na kile kilichopigiwa kura na wananchi.

Trump amesema kuwa alimshauri Bi.May njia nzuri ya kujiondoa kwenye umoja wa Ulaya lakini hakumsikiliza,hatuwezi kuwa tayari kuwa na mashirikiano ambayo ndani yake kuna umoja wa Ulaya.

Mhariri wa BBC wa masuala ya siasa Laura Kuenssberg, amesema kauli hii ya Trump inatupilia mbali madai ya Bi May ambaye amekuwa akisema Uingereza bado inaweza kuwa na makubaliano imara ya kibiashara na dunia pamoja na kuwa na ushirikiano kwa namna moja na umoja wa Ulaya.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad