Waislamu wenye msimamo mkali wahukumiwa kunyongwa


Mahakama nchini Misri imewahukumu kifo Waislam 75 wenye msimamo mkali wakiwemo viongozi wa kikundi kilichopigwa marufuku cha Muslim Brotherhood hukumu inayoelezwa ni kubwa kutolewa mara moja kwa watu wengi nchini humo. 

Hata hivyo sheria nchini Misri zinataka Mufti Mkuu aridhie au kukataa kutekelezwa kwa hukumu hiyo na pia waliohukumiwa wana haki ya kukata riufaa. 

Waliotiwa hatiani ni miongoni mwa washitakiwa 713 waliofunguliwa mashitaka ya madi ya kuwauwa askari polisi  katika mapambano baina ya vikosi vya usalama na  wafuasi wa aliyekuwa Rais wa Misri, Mohamed Morsi aliyeondolewa madarakani mwaka 2013. 

Wanachana waandamizi wa Muslim Brotherhood, Mohamed El-Baltagui, Issa Aryan na Safwat Hijazi walikuwepo mahakamani wakati hukumu ikitolewa  wakati wengine 31  wamehukumiwa wakiwa hawapo mahakamani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad