Zitto Afunguka Kuondoka Kwa Waitara Chadema na Kujiunga CCM


Baada ya Mbunge wa Ukonga (Chadema) Mwita Waitara kutangaza kurudi CCM, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe  ametoa neno kuhusu hatua hiyo. Anaripoti Regina Kelvin

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Zitto amemhoji Mwita kwa kuandika kuwa, amerudije CCM wakati viongozi waandamizi wa Chadema wana kesi mahakani  huku Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu yuko hospitalini takribani mwaka kwa majeraha ya risasi kutokana na jaribio la kuuawa.

“Mbunge mwenzio yupo hospitali mwaka sasa kwa majeraha ya risasi kufuatia jaribio la kumwua. Viongozi wa Chama chako Karibu wote Ngazi ya Taifa wana kesi inayohatarisha kuwaweka jela. Watu wanauwawa na kupotea kila siku. Halafu unajiunga na hao wanaosababisha hayo? Kweli Mwita?” amehoji Zitto.

Waitara ametangaza uamuzi wa kurudi CCM mchana wa leo jijini Dar es Salaam mbele ya wanahabari baada ya kukaribishwa rasmi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Hunphrey Polepole.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad