Aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi la Uganda Kale Kayihura Ashtakiwa

Aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi la Uganda Kale Kayihura Ashtakiwa
Aliyekuwa Mkuu wa jeshi la polisi nchini Uganda IGP - Kale Kayihura amefikishwa katika mahakama ya jeshi ya Makindye kwa mashtaka kadhaa dhidi yake.

Ameshtakiwa kwa kushindwa kulinda zana za kivita.

Kwamba kati ya mwaka 2010 na 2018 alitoa idhini silaha zitolewe kwa watu wasiostahili, na ameshtakiwa kwa kusaidia na kuhamishwa kiharamu kwa raia wa Rwanda walio uhamishoni.

Kayihura amekana mashtaka yote matatu.

Mawakili wake wameomba aachiliwe kwa dhamana, na wakatakiwa wawasilishe ombi hilo kwa maandishi.

Bobi Wine ashtakiwa kwa uhaini Uganda

Alikamatwa nyumbani mwake katika kijiji cha Katebe wilayani Lyantonde district mnamo Juni na amekuwa kizuizini kwa miezi miwili kufikia sasa.

Jenerali Kale Kayihura, ambaye kwa wakati mmoja aliyekuwa mojawapo ya watu wenye nguvu nchini Uganda amekuwa akizuiliwa katika kambi ya kijeshi huko Makindye, kitongoji cha mji mkuu Kampala.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad