Baba Dimpoz-Natamani Kwenda Kumuona Mwanangu Sauzi

Baba Dimpoz-Natamani Kwenda Kumuona Mwanangu Sauzi
Baba mzazi wa Msanii wa Bongo fleva Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz, Faraji Nyembo amefunguka na kudai anatamani sana kuenda nchini Africa ya kusini  kwenda kumuona mtoto wake.

Ommy Dimpoz amekuwa nchini Afrika ya Kusini kwa Miezi kadhaa kwa ajili ya matibabu anayopata baada ya kufanyiwa opersheni Miezi michache iliyopita.

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa, Baba Dimpoz amesema anatamani sana kwenda kumuona mwanaye Afrika Kusini alipo kwa matibabu lakini anashindwa kutokana na kwamba hana nauli ya kufika huko.

Namuombea mwanangu usiku na mchana ili Mungu amponye arudi kwenye muziki kama kawaida na kwa uwezo wake atapona, pia natamani sana kwenda kumuona lakini sina uwezo na naamini angeshangaa na angefurahi sana kuniona.

Ommy Dimpoz na Baba yake hawana uhusiano mzuri kwani siku za nyuma Mzee Nyembo ambaye anaendesha bajaji aliwahi kumtuhumu Dimpoz kwa kumtelekeza Kwenye maisha magumu na yeye Kula bata nje ya nchi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad