Barakah The Prince Ajibu Tuhuma Za Kuwa na Kiburi


Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefungukia tuhuma ambazo amekua akirushiw ili nyingi kuwa ana kiburi.

Mashabiki wengi wa muziki wa Bongo fleva wamekuwa wakimtuhumu Barakah The Prince kwa kudai kuwa ni mtu ambaye ana kiburi hasa kwa mashabiki wake.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Barakah amefunguka kuwa yeye sio mfuatiliaji mzuri wa comments za mashabiki wake kwenye mitandao ya kijamii na kuhusu madai ya kuwa ana kiburi ameeleza kuwa wanamkosea sana Mwenyezi Mungu kwani wanaamini vitu ambavyo hawaambiwa bila kuthibitisha.

Mimi sio msamaha sana wa comments za mashabiki maana naamini ukisikiliza maoni ya watu unaweza ukachanganyikiwa mwisho wa siku unatakiwa ufabye kitu ambacho unajua kitakuwa Kiba faida kwako kuliko kufuata matakwa ya watu.

Unajua watu wanaamini wanachokisikia kuna kundi Dogo la watu linalowaaminisha watu wengi kuwa mimi mjeuri jambo ambalo sio la kweli kwani mashabiki wangu wa kweli wanajua mimi siko hivyo kabisa”.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad