Barnaba: Fuatilieni Mziki Wangu na si Maisha Yangu Binafsi

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barnaba amemfungukia skendo zinasambaa Kwenye mitandao ya kijamii na kusema anataka mashabiki zake wasikilize miziki yake badala ya skendo zake.

Wanawake wawili wamekuwa Kwenye vita ya mitandao ya kijamii dhidi ya penzi la Barnaba ambapo amekuwa Kwenye Mahusiano na wanawake hao kwa wakati mmoja.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Enews cha EATV Barnaba amekataa skendo hizo na kudai hazina ukweli wowote na kuwataka mashabiki zake wasizitilie maanani:

Hizo skendo mimi nazisikia tu kama wewe kwa maana hazina ukweli Kwanza mimi sio mtu wa kuanika mahusiano yangu mitandaoni kwaiyo tafadhali mashabiki zangu msisikilize kelele za watu hao. Bali naombeni msikilize mziki wangu na kazi zangu”.

Lakini pia Barnaba anafanya vyema na  wimbo wake mpya unaoitwa Tuachane mdogo mdogo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad