Breaking News: Mahakama ya Jeshi Nchini Uganda Yamuondolea Mashtaka Bobi Wine Aachiwa Huru

Taarifa za hivi punde kutoka Uganda ni kwamba mahakama ya jeshi imemuondolea mashtaka mbunge wa Kyadondo Robert Kyagulanyi.

Inaarifiwa kwamba mahakama hiyo ya jeshi inataka badala yake inataka kumkabidhi mbunge huyo kwa mahakama ya kiraia ajibu mashtaka ya uhaini pamojana wabunge wengine waliokamatwa.

Mbunge huyo ambaye aliwahi kuwa mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bobi Wine leo alitarajiwa kurudishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.

Mawakili wake awali walijuzwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakozuiliwa mjini Kampala.

Kumekuwa na shinikizo kubwa kimataifa la kutaka Bobi Wine aachiwe huru.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad