Daimond, Mboso Awakamatiki Kenya..... Wawazidi Sauti sol, Drake Washika Namba Moja Kenya iTunes Top Songs

Daimond, Mboso Awakamatike Kenya..... Wawazidi Sauti sol, Drake  Washika Namba Moja Kenya iTunes Top Songs
Wasanii kutokea lebo ya WCB wanaonyesha kufanya vizuri katika chart za iTunes nchini Kenya.

Wasanii hao ni Mbosso na Diamond Platnumz ambapo wapo katika nafasi tano za juu wakishindana na wasanii wengine kama Drake na Sauti Sol.

Wimbo wa Diamond Platnumz (WCB Wasafi) uitwao Jibebe ambao amewashirikishwa Mbosso na Lava Lava unashika nafasi ya kwanza kwenye chart hiyo.

Huku Mbosso akiingiza nyimbo mbili katika ile top five, wimbo wake Nadekezwa upo nafasi ya nne na ngoma Nipepe nafasi ya tano.

Diamond Platnumz, Mbosso na Lava Lava kwa sasa wanafanya vizuri na wimbo wao Jibebe ambapo hapo jana ndipo walitoa video ya wimbo huo ambayo imefanyika nchini Afrika Kusini na Director Justin Campos.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad