Familia za Korea Kaskazini na Kusini zilizotenganishwa na vita zakutana kwa mara ya kwanza

Familia za Korea Kaskazini na Kusini zilizotenganishwa na vita zakutana kwa mara ya kwanzaKundi la watu wazee kutoka Korea Kusini kwa sasa wako nchini Korea Kaskazini kukutana na jamaa zao wenye hawajawaona tangu vimalizike vita vya mwaka 1950-1953.

Vita hivyo vilisababisha rasi ya Korea kutengana na watu waliokuwa wanaishi upande wa Kaskazini wasikuwe na uwezo wa kuondoka.

Korea hizo mbili ambazo bado ziko kwenye mzozo wa vita, zilikuwa zimepanga shughuli ya kuwakutanisha watu hao awali lakini shughuli hii ndiyo ya kwanza kwa miaka mitatu.

Korea Kaskazini 'inaunda makombora mapya'
Watu kutoka nchini Korea walichaguliwa mwa mfumo wa bahati nasibu huku mtu mzee zaidi katia kundi hilo akiwa wa umri wa miaka 101.

Kuna raia 83 wa Korea Kaskania na 89 wa Korea Kusini wanaoishukia katika shughuli hiyo ya kukutana.

Watu 100 walikuwa wamechaguliwa kutoka kila upande lakini wengine waliondoka baada ya kufahamu kuwa jamaa zao waliokuwa na matumaini ya kuwaona hakuwa hai tena.

Mwanamke mmoja mweny miaka 92 aliwaambia waandishi wa habari kuwa alikuwa anaenda kumuona mtoto wake wa kiume kwa mara ya kwanza tangu vita vimalizike.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad