Harmonize Aeleza Namna Kwangwaru inavyotikisa Kenya


Msanii wa muziki Bongo, Harmonize ameeleza jinsi wimbo wake, Kwangwaru ulivyomkubwa nchini Kenya.

Muimbaji huyo kutokea WCB kwa sasa anafanya tour nchini humo. Katika show  anazofanya inaonyesha kuwa na muitikio mkubwa sana wa watu kuhudhuria.

Harmonize ameeleza katika show yake ulipofika wakati wa kuimba Kwangwaru mashabiki hawakutaka aimbe hata kidogo badala yake wao ndio waimbe.

Ameongeza kuwa hata baadhi ya watu nchini humu wamemueleza kuwa Kwangwaru ndio wimbo wa mwaka, yaani uliofanya vizuri zaidi.

Wimbo Kwangwaru ambao Harmonize amemshirikisha Diamond Platnumz hadi sasa una views Milioni 23 katika mtandao wa YouTube ukiwa na miezi minne tangu ulipotoka na kuwa wimbo wa kwanza wa msanii huyo kufikisha idadi hiyo ya views.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad