Harmonize Ajibu Tuhuma za TID kuhusu kukopi muziki wa Nigeria


Msanii wa muziki Bongo, Harmonize amejibu tuhuma zilizotolewa na TID kuwa amekuwa akiinga muziki wa Kinigeria na kusahau Bongo Fleva.


Muimbaji huyo kutokea WCB akipiga stori na Wasafi TV amesema TID hakuwa ana mlenga yeye bali kuna watu alikuwa anataka kuwafikishia ujumbe huo.


"Mimi nafikiri TID ni kaka kabisa, ana namba yangu na nina yake pia, nadhani hakuwa ananilenga mimi kwa sababu angekuwa ana nilenga mimi  alikuwa ana uwezo wa kunipigia na kuniambia mdogo wangu hii haipo sahihi, usiimbe hivi," amesema.


"Naamini kuna watu alikuwa anawalenga lakini ili asiingie matatizoni na wasanii wengine akaona acha nipitie njia ya mdogo wangu Harmonize," amesema Harmonize.


Harmonize kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Atarudi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad