Je Kuwa na Watoto Wengi ni Baraka Au Mzigo?

Je Kuwa na Watoto Wengi ni Baraka Au Mzigo?
Katika jamii nyingi za kiafrika, kupata watoto ni jambo linalochukuliwa kama baraka. Baadhi ya jamii huchukulia kuwa na watoto wengi kama ishara ya utajiri na fahari. Ni jambo ambalo pia hupigiwa chapuo.

Nchini Ghana, wenyeji wa kiasili wa Mji Mkuu wa Accra ni kabila la Ga, mwanamke anapojifungua mtoto wake wa 10 huzawadiwa kondoo mzima. Desturi hiyo hufahamika "nyongmato".

Ukizunguka Jijini Accra leo, kwenye mabenki, vyombo vya usafiri, mitaani na kwengineko ni nadra kukutana na mama mwenye watoto zaidi ya wanne. Yawezekana Accra sio sehemu sahihi tena ya kutafuta familia yenye watoto 10 na kuendelea.

Miezi miwili iliyopita mwandishi wa BBC nchini Ghana Elizabeth Ohene alihudhuria mazishi ya rafikiye wa toka shule ya msingi ambaye ameacha familia ya watu 44. Marehemu ameacha watoto nane,wajukuu 26 na vitukuu 8.

Tanzania yawafungulia kesi kijiji kizima kwa kosa la kuharibu miundombinu
Uzazi usiopangwa na ongezeko kubwa la watu ni moja ya sababu kuu inayotajwa kuchochea umaskini barani Afrika.

Nchi ya Ghana ilikuwa na watu milioni 5 wakati ikipata uhuru mwaka 1957, miaka 60 baadae leo hii kuna watu milioni 30. Norway katika kipindi hichohicho wametoka kuwa na watu milioni 3.5 mpaka milioni 5.3.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad