Kitendo Cha Diamond Kumuita Mobetto Mchepuko Chamliza Mama Hamisa


Siku chache zilizopita staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz aliwaacha watu midomo wazi baada ya kufanya Interview na Kwenye Interview hiyo kumuita Hamisa Mchepuko.

Kwenye clip hiyo ya Diamond inayodaiwa kuwa ni mahojiano yake aliyoyafanyia nje ya nchi, Diamond alisikika akijilaumu kuwa mwaka 2017 ulikuwa mbaya maishani kutokana na matukio mabaya yaliyomtokea. Alisema, mwaka huo ndiyo ambao aligombana na mpenzi wake wa muda mrefu, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ aliyezaa naye watoto wawili, mmoja wa kike.

Alisema hayo yote yalitokea baada ya kuchepuka na Mobeto na kujikuta amempa ujauzito na hata Zari alipojaribu kuhoji baada ya kusikiasikia fununu, alijaribu kumficha ili kulinda uhusiano wake, lakini hata hivyo jipu lilikuja kupasuka baada ya Mobeto kuvujisha picha zao wakiwa kimahaba chumbani, jambo ambalo lilimharibia sana.

Baada ya clip hiyo kusambaa mashabiki wa Hamisa walimjia juu Msanii huyo na kumtuhumu kwa tabia mbaya ya kudhalilisha wanawake hasa ambao amekwisha zaa nao.

Baada ya sakata hilo Global Publishers lilimsaka mama mzazi wa Hamisa Mobetto, Shufaa Lutiginga ambaye alionyesha kutofurahishwa na Kauli hizo za mkwewe  dhidi ya mwanaye Mobetto:

Jamani inauma na kwa kweli nisingependa hayo mambo jamani kuyaongelea mimi… jamani naombeni sana mtafuteni huyo mwenyewe aliyesema au Mobeto tafadhali, niacheni mimi nipumzike”.

Lakini pia Kwenye Interview hiyo  Diamond alisikika akiwaasa vijana wote wenye wapenzi wao ‘serious’ au wenye wake zao, kuwa makini pindi wanapokuwa na michepuko ili kuepuka kupata watoto wa mchepuko kama ilivyomtokea yeye, jambo ambalo limekuwa baya maishani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad