Nina Kipaji Ndomana Nimejiunga na Coastal Union- Alikiba

Nina Kipaji Ndomana Nimejiunga na Coastal Union- Alikiba
Staa wa Muziki wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguka na kuongelea kitendo chake cha kujiingiza katika soka la kulipwa ambapo hivi sasa ni mchezaji rasmi wa Coastal Union.

Wiki chache zilizopita Ali kiba alitangazwa rasmi kama mchezaji wa timu ya Coastal Union yenye makazi yake mkoani Tanga.

Kwenye mahojiano na Azam Tv, Ali Kiba anafunguka juu ya njia mpya aliyochukua na kueleza kuwa ana kipaji cha kucheza mpira na uwezo pia anaamini kuwa anao:

Mimi kwa kipaji changu binafsi nimeona kwamba ninaweza na ndio maana nikajiunga na Coastal Union sababu ya kipaji nilichokuwa nacho”.

Lakini pia ALi Kiba amefunguka kuhusu uwezo wa timu yake hiyo mpya na malengi waliyokuwa nayo:

Coastal Union wanajutahidi na ni wapambanaji na tunatafuta title msimu huu japokuwa kuna timu kongwe lakini mpira wanasemaga unadunda kwaiyo ni kupambana tu tutafika”.

Ali Kiba pia ameweka wazi kuwa kinywaji chake cha Mo Faya ndiyo kitaidhamini timu hiyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad