Pazia la Ligi Kufunguliwa Leo..... Simba na Tanzania Prisons Kuonyeshana Ubabe

Pazia la Ligi Kufunguliwa Leo..... Simba na Tanzania Prisons Kuonyeshana Ubabe
Kikosi cha Simba kianshuka dimbani leo majira ya saa moja jioni kuanza rasmi pazia la Ligi Kuu Bara kwa kucheza na Tanzania Prisons.

Kuelekea mchezo huo Simba itawakosa wachezaji wake watatu ambao ni Mlinda mlango Deogratius Munishi 'Dida', Kiungo Clatous Chama na Mganda Emmanuel Okwi.

Dida na Chama watakosekana katika mchezo huo kutokana na kukosa Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ambazo mpaka sasa bado hazijawasili.

Aidha, Mganda, Emmanuel Okwi naye atakosekana baada ya kuumia katika mchezo wa Ngao ya Hisani uliopigwa jijini Mwanza Agosti 18 ndani ya dimba la CCM Kirumba.

Simba itaanza pazia la michuano hiyo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam majira ya saa moja za usiku ili kuwapa nafasi watazamaji kufurahia sikukuu ya Eid uzuri zaidi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad