Rais wa Liberia Kaamua Kumpa Tuzo Arsene WengerA

Rais wa Liberia Kaamua Kumpa Tuzo Arsene WengerA
Rais wa Liberia George Weah Jumanne ya August 21 2018 ameripotiwa kuwa ameandaa tuzo kwa kocha wa zamani wa club ya Arsenal ya England Mr Arsene Wenger.

George Weah amemualika kocha Arsene Wenger, Liberia katika jiji la Monrovia kwa ajili ya kumpa tuzo ya heshima kwani ni kocha ambaye amefanikisha yeye kufikia mafanikio aliyonayo sasa hivyo anaamini anastahili tuzo ya heshima.

Kama ufahamu George Weah ambaye ni Rais wa Liberia kwa sasa amewahi kufundishwa soka na kocha Arsene Wenger mwaka 1998 wakati alipomsajili katika club ya Monaco ya Ufaransa.

Weah ambaye anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji pekee wa Afrika kuwahi kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Dunia 1998, alistaafu soka mwaka 2003 na kuingia rasmi katika siasa, hivyo Ijumaa hii nchini Liberia, Wenger atakuwepo kukabidhiwa tuzo ya heshima.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad