Sababu 2 za Jackline Wolper kutoswa shindano la Miss Tanzania


Hatimaye imebanika sababu ya Jackiline kutoswa kwenye kamati ya Majaji ya Miss Tanzania kwenye fainali ya mashindano yaliyofanyika Kanda ya Ziwa hivi karibuni.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo August 27, 2018 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya The Look inayosimamia Mashindano hayo, Basilla Mwanukuzi ameleza sababu za Wolper kutolewa.

"Katika ngazi ya kanda Majaji ni kamati ya Miss Tanzania au watu ambao kamati itapendekeza, sasa Wolper sio kamati ya Miss Tanzania," amesema.

"Lakini pia Majaji wanapewa semina, Wolper alichelewa kufika kwenye semina, ataingiaje kujaji hajaongozwa?. Sio tu uwe super star  uje kujaji, hapana! kuna miongozo maalumu alitakiwa awahi ahudhurie semina ambayo wale Majaji wengine walipewa, yeye kafika semina imeshaisha," amesema  

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad