Serena Williams Ndiye Mwanaspoti Mwanamke Mwenye Kipato cha Juu Zaidi

Serena Williams Ndiye Mwanaspoti Mwanamke Mwenye Kipato cha Juu Zaidi
Nane kati na wanaspoti 10 wa kike matajiri zaidi ni wa tenisi, huku bingwa mara 23 wa Grand Slam Serena Williama akichukua nafasiu ya kwanza kwenye Forbes.

Williams alilipwa dola 62,000 mwaka uliopita baada ya kuwa nje kwa miezi 14 kujifungua lakini alijizolea dola milioni 18 kutoka kwa matangazo ya biashara.

Mchezaji wa Badminton PV Sindhu na mwendesha magari Danica Patrick ndio wanaspoti wasio wachezaji tenisi walio katika orodha ya kumi bora.

Mwezi Juni Forbes iliwaorodhesha wanaspoti 100 wenye kipato cha juu zaidi lakini hakukuwa na mwanamke kwenye orodha hiyo baada ya Williama kukosa kuorodheshwa.

Mwanamasumbwi Mmarekani Floyd Mayweather alichukua nambari moja akifuatwana mchezaji soka Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Mapato ya Williams yanamweka nafasi ya kwanza kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Caroline Wozniacki yuko nafasi ya pili baada ya kushinda ubingwa wa Grand Slam kwenye mashindano wa Australia Open, ushindi uliompa dola milioni 3.1 na kuongeza kipato chake hadi pauni milioni 13.

Rais wa Urusi Sharapova alikuwa mwanaspoti wa kike aliyekuwa na kipato cha juu zaidi kwa miaka 11 mfululizo lakini kipato chake kimeshuka kufuatia marufuku ya miezi 15.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad