Watuhumiwa Sugu wa Unyang'anyi wa Kutumia Silaha Wakamatwa

Watuhumiwa Sugu wa Unyang'anyi wa Kutumia Silaha Wakamatwa
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia watuhumiwa sugu 13 kwa tuhuma za unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali ya jiji na mikoa ya jirani.

Watuhumiwa hao ni BALIZANILA EZEKIEL (37) Raia wa Burundi, SHUKURU HASSAN (38), SAIDI SHABANI (34) HAJI SALUM (38) FRENK KALIKENE (32) na wengine 8.
Watuhumiwa hao wamekuwa wakiendelea na vitendo vya uhalifu wa kutumia silaha licha ya kuachiwa huru baada ya kumaliza vifungo vyao katika magereza mbalimbali hapa nchini.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na bostola aina ya Chinese star iliyokuwa na risasi nne ndani ya magazine, pamoja na risasi nyingine tisa zikiwa zimehifadhiwa pembeni.
Oparesheni hii ni endelevu ya kupambana na wahalifu wote wanaofanya unyang’anyi ndani ya jiji la Dar es salaam na wanaokuja kujificha jijini Dar es salaam baada ya kufanya uhalifu kutoka mikoa ya jirani.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad