Wema Sepetu amemjibu Zari ? ‘Siendi kwenye party ya Tiffah SA


Leo ni siku ya kuzaliwa ya mtoto wa Diamond Platnumz, Princes Tiffah ambapo wadau mbalimbali wamemtumia ujumbe wa siku yake ya kuzaliwa kupitia mitandao ya kijamii.

Wema Sepetu ambaye alikuwa mpenzi wa zamani wa Diamond amesema hawezi kwenda Afrika Kusini kwenye party ya mtoto huyo kama walivyoalikwa Diamond Platnumz.

“God Bless The Next Big Thing… Like Father Like Daughter. On August 6th, A Star was Born… 🙏🏼🙏🏼🙏🏼. Msije mkadhani kwenye Party naenda. Wala siendi. I jus wished the lil angel Dats it…!!! 😌😌😌 #SinagaHianaMie . Maana hamkawii,”

Kauli hiyo imekuja baada ya Zari kudaiwa kutoka kauli kupitia mitandao ya kijamii kwamba hataki ugeni wa waalikwa hao wa Diamond akiwemo Wema Sepetu ambaye alialikwa kupitia kamati ya maandali ya arobaini ya Zamaradi.

Kupitia sherehe ya arobaini ya mtoto wa Zamaradi, Babu Tale kwa niaba ya WCB walitangaza kuwapeleka wanakamati wao akiwemo Wema Sepetu nchini Afrika Kusini ili Tiffah asherekee siku yake ya kuzaliwa akiwa shangazi zake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad