Afungwa Jela Miaka 30 Kwa Kumbaka Mlemavu wa Akili Ambaye pia ni Bubu


Mahakama ya Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi imemuhukumu kifungo hicho Ramadhani Shaban(24) mkazi wa Majengo B kwa kumbaka mlemavu huyo wa miaka 15

Hukumu hiyo imetolewa jana Septemba 18 na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Gasper Luoga baada ya mshitakiwa kukiri kutenda kosa hilo

Mwanasheria wa Serikali mkoani humo, Flaviana Shio alidai Mahakamani hapo kuwa Shabani alitenda kosa hilo Septemba 9 saa 12:00 jioni katika mtaa wa Majengo B.

Mshtakiwa anadaiwa kufanya kitendo hicho kwenye chumba chake alichopanga ambapo baada ya tukio hilo mlalamikaji alitoka nje na kuanza kuwaonesha watu ishara kuwa amebakwa
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad