Aikah na Nahreel Washeherekea Miaka Kumi Ya Mahusiano

Aikah na Nahreel Washeherekea Miaka Kumi Ya Mahusiano
Wasanii wanaounda kundi la Navy Kenzo ambao wamehusika kutoa hit songs kama Game na Kamatia chini,Producer Nahreel na Aikah Mareale wanasheherekea miaka kumi ya Mahusiano.

Baada ya kuwa Kwenye Mahusiano kwa miaka kumi Nahreel na Aikah  tayari wamejaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume mapema mwaka huu anayeitwa Gold.

Wasanii hao walikutana miaka kumi iliyopita nchini India ambapo wote walikuwa wameenda kimasomo na kuanzisha Safari yao ya mapenzi pamoja na kufanya Muziki pamoja.

Pamoja na kuwa wote kwa miaka kumi sasa wasanii hao wameweka wazi kuwa hawana haraka ya kufunga ndoa kwa sababu tu maneno ya watu bali watafunga ndoa pale watakapokuwa tayari.

Wapendanao hao wameonekana wakila bata katika viwanja mbali mbali katika visiwa vya Zanzibar na hata kuandikiana posti za kimahaba Kwenye mitandao ya kijamii:

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad