Baba Mzazi Ommy Dimpoz: Mwanagu Akiona Naenda Kumjulia Hali Sauz Angefurahi Sana Kuniona Tatizo Sina Nauli

Baba Mzazi Ommy Dimpoz: Mwanagu Akiona Naenda Kumjulia Hali Sauz Angefurahi Sana Kuniona Tatizo Sina Nauli
Baba mzazi wa Msanii wa Bongo Fleva Omary Nyembo maarufu kama Ommy  Dimpoz, Faraji Nyembo amefunguka na kudai kuwa anatamani kwenda nchini Afrika ya Kusini kumuona mtoto wake ambaye anaendelea kupatiwa matibabu huko baada ya kufanyiwa upasuaji.

Akizungumza na www.eatv.tv Baba Ommy amesema kuwa anatamani kwenda Afrika Kusini lakini kwa sasa hawezi kutokana na kukosa nauli ya kumfikisha huko hivyo basi kuendelea kumuombea akiwa nchini.

''Namuombea mwanangu usiku na mchana ili Mungu amponye arudi kwenye muziki kama kawaida na kwa uwezo wake atapona, pia natamani sana kwenda kumuona lakini sina uwezo na naamini angeshangaa na angefurahi sana kuniona'' amesema baba wa Ommy.

Amekiri kuwa hawana mahusiano mazuri na mwanae kutokana historia ya huko nyuma kuna mambo yalitokea ambayo ni yakifamilia ndio maana yeye na mwanae walifikia hatua hiyo.

Ommy amekuwa akisumbuliwa na tatizo la koo la chakula ambalo liliziba hali iliyopelekea ashindwe kupitisha chakula wala maji, kwa mujibu wa madaktari tatizo hilo limetokana na sumu ambayo inasemakna Ommy alikula  bila kutambua.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad