Binti Amfanya Rais Magufuli Achangishe Fedha

Akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika mikoa ya kanda ya ziwa ambapo kwasasa yupo Mkoani Mara Rais Magufuli, leo ameendesha harambee ndogo katika eneo la Nyamongo ya kuchangia fedha kwa ajili ya kutatua kero katika shule ya Ingwe, huku akiwataka wanaume katika eneo hilo kuacha mawazo


Akiongea na wananchi katika eneo hilo la Nyamongo wilayani Tarime mkoani Mara, Rais alimruhusu binti aitwaye Monica Bernad mwanafunzi wa kidato cha tano, katika shule ya Ingwe kueleza kero zilizopo katika shule hiyo ya Upili, ambapo alitaja kero kadhaa kama upungufu wa mabweni na madarasa.

''Kwanza Monica nikushukuru sana lakini si ajabu vijana wa kiume wa Nyamongo wameshaanza kumwangalia angalia na pengine kufikiria kumtorosha, washindwe kabisa wasimsogelee Monica ambaye ameongea kwa niaba ya wanafunzi na vijana wengi'', alisema Magufuli.



Mwanafunzi Monica Bernad kushoto na Rais Magufuli kulia kwenye mkutano leo Nyamongo

Aidha katika kutatua kero za shule hiyo Rais aliendesha harambee ndogo katika mkutano huo wa hadhara ambapo viongozi mbalimbali wakiwemo Madiwani, Wabunge na Mawaziri walichangia na kuwezesha kupatikana kwa takribani shilingi milioni 24.

Mwisho Rais Magufuli yeye alichangia kiasi cha shilingi milioni 5, hivyo kufikisha zaidi ya milioni 29 ambazo amewaagiza Mkuu wa mkoa na RPC kuhakikisha zinakusanywa na kwenda kutumika kama ilivyokusudiwa ili wanafunzi katika shule ya Ingwe wasome bila shida.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad