Emmanuel Mbasha Aitamani Ndoa Adai Yeye ni Husband Material

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Emmanuel Mbasha bado anaonekana kusumbuliwa na swala la kutamani ndoa pamoja na kwamba aliwhikuoa hapo awali na kuachana na mke wake kwa talaka na mke wake kuolewa na mwanaume mwingine.

Emmanuel Mbasha amekuwa akiandika baadhi ya maneno ya kuonyesha kuwa kwa sasa anaona kuwa hata yeye yuko tayari kwa ndoa licha ya hapo awali alisema anahitaji muda na hata kusema kuwa tangu kuachana na mke wake kwa sasa hana mahusiano tena.

Katika moja ya posti zake za hivi karibuni, Emmanuel aliandika maneno yenye kuonyesha kujinadi na kusema kuwa yeye ni moja ya wanaume wenye sifa za kuoa na kwamba mwanamke atakae muoa atakuwa anafaidi sana kutokana na sifa zake

“Mungu ni fundi sana anajua kufanya kazi kwa ustadi mkubwa na wala hakosei,… cheki nilivyo tall, handsome, white, mwili umependeza,  pamba ya aina yoyote ile nina damshi  na sura ya ki-star….Asante baba kwa mibaraka yote ulinijalia  na atakae kuja kuolewa na mimi atakuwa na bahati sana  na wala hatokuja kujuta kwa sababu mimi ni husband material.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad