Hamisa Mobetto Hakamatiki Awaacha Mbali Maua Sama , Aslay na Mbosso

Hamisa Mobetto Hakamatiki Awaacha Mbali  Maua Sama , Aslay na Mbosso
Msanii wa Bongo fleva na mwanamitindo maarufu Hamisa Mobetto amezidi kufanya vyema katika ulimwengu wa muziki baada ya video yake kushika namba moja Kwenye mtandao wa Youtube.

Hamisa Mobetto ambaye ndio kwanza ametoa Single yake ya kwanza inaitwa ‘Madam Hero’ ameonekana kung’aa mara baada ya video yake hiyo kufanya vyema zaidi.

Mpaka muda huu video hiyo inatrend namba moja Kwenye mtandao wa kijamii wa Youtube kwa Tanzania na kukimbiza video za wasanii wakali wanaofanya vizuri nchini kama Mbosso na ngoma yake ya Hodari, Aslay na wimbo wake wa Kwatu na Maua Sama na kiokote.

Hii sio mara ya kwanza kwa Mobetto kusikika akiimba ameshasemekana kuweka vocal Kwenye ngoma ya Jibebe ya Diamond Platnumz.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad