Hamisa Mobetto "Nilipoanza Mapenzi na Diamond Hakuwa na Pesa wala Huo Mwili Alionao Sasahivi"



Mwanamitindo na Msanii wa Bongo fleva Hamisa Mobetto amefunguka Tena na kumuongelea aliyekuwa mpenzi wake na Baba watoto wake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Kwenye mahojiano aliyofanya siku ya jana kwenye Chipukeezy Show nchini Kenya, Hamisa aliulizwa alivutiwa nini hasa kwa Diamond kama ilikuwa ni Sura, Mwili wake, Pesa au umaarufu?

Hamisa alifunguka:

Siwezi kusema kiukweli kipi kilichonivutia kwa Diamond kwa sababu mimi na yeye tulipokutana kwa mara ya kwanza hakuwa na hivyo vitu vyote unavyovitaji yaani hakuwa na pesa, hakuwa na mwili aliokuwa na sasa hivi wala hakuwa na umaarufu”.

Lakini pia Hamisa ameweka wazi kuwa aliamua kumuacha Diamond kwa sababu alihisi kabisa ulikuwa wakati sahihi kwake yeye kuendelea na maisha yake kwa sababu anaamini kuna wanaume wengine wengi kwa ajili yake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad